Thursday 5 June 2014

TFF kusikiliza rufaa ya Wambura















SAKATA la Uchaguzi Mkuu wa Simba limeingia katika hatua nyingine ambapo Kamati ya rufani ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) inaketi Jumatatu ya Juni 9, mwaka huu kusikiliza rufani iliyowekwa na Michael Wambura.
Rufani hiyo iliwekwa na Wambura aliyekuwa anawania nafasi ya makamu wa rais kupinga kuondolewa kwake katika kinyang’anyiro hicho na Kamati ya Uchaguzi ya Simba.
Wambura anapinga kuondolewa katika nafasi hiyo kutokana kwa sababu ya kutokidhi vigezo vya kugombea ikiwemo kutokuwa mwanachama wa Simba.
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi ya TFF inayoongozwa na Wakili Julius Lugaziya itakutana saa 5, asubuhi kwenye Hoteli ya Courtyard iliyopo Upanga, jijini Dar es Salaam kujadili rufani hiyo na kutoa matokeo.
Wakati huohuo, wachezaji wawili Ali Shabani Mabuyu na Juma Yusuf waliochaguliwa kwenda kwenye kambi ya Copa Coca-Cola ya Dunia nchini Brazil jana wamekabidhiwa bendera tayari kwa safari hiyo.

No comments:

Post a Comment